Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Ndege za Israel zakiuka tena anga ya Lebanon

Ndege za kijeshi za utawala haramu wa Israel kwa mara nyingine tena zimekiuka anga ya Lebanon. Jeshi la Lebanon limetangaza katika taarifa yake kwamba, ndege za kivita na za kijasusi za Israel zimepaa katika anga ya Lebanon kusini mwa nchi hiyo na katika maeneo mengine ya nchi hiyo. Taarifa ya jeshi la Lebanon imebainisha kwamba, hatua hiyo ya jeshi la utawala haramu wa Israel, kwa mara nyingine tena imekiuka wazi mamlaka ya kujitawala ya Lebanon na kupuuza pia azimio nambari 1701 la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. 
Serikali ya Lebanon imelaani mara chungu nzima hatua za jeshi la Israel za kukiuka mara kwa mara anga na mamlaka ya kujitawala nchi hiyo ya Kiarabu.

No comments: