Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Zarif: Tutaendelea na mazungumzo ya nyuklia

Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, Tehran itaendelea na mazungumzo yake na kundi la 5+1 lakini wakati huo huo itatoa majibu yanayofaa kwa vitendo vyote visivyo sahihi vinavyofanywa na madola ya Magharibi.
Muhammad Javad Zarif amesema hayo leo katika ukurasa wake wa Facebook na kusisitiza kuwa, Iran itaendelea na mazungumzo hayo kwa nguvu zake zote na itatoa majibu yanayofaa kwa hatua yoyote isiyo sahihi inayochukuliwa na dola lolote lile.

Ikumbukwe kuwa, siku ya Alkhamisi Wizara ya Hazina ya Marekani iliyawekea vikwazo vipya mashirika na maafisa kadhaa wa Iran kwa madai kuwa wamesaidia maendeleo ya nyuklia ya Iran.
Vikwazo hivyo vipya vya Marekani vimekuja licha ya Iran na kundi la 5+1 linaloundwa na nchi za Russia, China, Ufaransa, Uingereza, Marekani pamoja na Ujerumaini kutiliana saini makubaliano ya nyuklia Novemba 24 mwaka huu mjini Geneva Uswisi ambayo kwa mujibu wake, pande zote zilitakiwa kujenga hali ya kuaminiana na kurahisisha njia za utekelezaji wa vipengee vya makubaliano hayo.

No comments: