Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Zarif: Iran imedhamiria kufikia makubaliano ya mwisho

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imedhamiria kufikia makubaliano kamili ya mwisho na kundi la 5+1. Muhammad Javad Zarif amesema Iran inafungamana na mchakato wa mazungumzo hayo na kuongeza kuwa Tehran itaendelea na mazungumzo ya nyuklia licha ya vizuizi vilivyojitokeza wiki iliyopita katika njia ya mazungumzo ya nyuklia ya Iran na kundi la 5+1.

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameyasema hayo katika mahojiano aliyofanya na David Ignatius, mwandishi wa gazeti la Washington Post. Washington Post limemnukuu Muhammad Javad Zarif na kuandika kuwa katika makubaliano ya mwisho, Iran itathibitisha kwamba miradi yake ya nyuklia inafanyika kwa malengo ya amani.
Wakati huo huo katika mahojiano yake na  kanali ya CBS, Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amevitaja vikwazo vya hivi karibuni vya Marekani dhidi ya shakhsiya kadhaa na makampuni ya Iran kuwa ni makosa makubwa na kueleza kuwa, Tehran hata hivyo itaendelea kuheshimu makubaliano ya muda iliyofikia na kundi la 5+1 kuhusu miradi yake ya kuzalisha nishati ya nyuklia. 

No comments: