Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

UN: Uturuki imepeleka tani za silaha nchini Syria

Ripoti iliyotolewa na Umoja wa Mataifa imesema kuwa Uturuki imepeleka zaidi ya tani 47 za silaha ili kuwaunga mkono waasi wanaopigana dhidi ya serikali ya Syria tangu mwezi Juni mwaka huu.
Ripoti hiyo imeeleza kuwa, mwezi Septemba pekee Uturuki iliwapelekea waasi wa Syria idadi tofauti za bunduki, ambapo kiwango kikubwa zaidi kilikaribia tani 29.
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Uturuki Levent Gumrukcu awali alikanusha takwimu hizo lakini baadaye alikubali akidai kwamba ripoti hiyo ya Umoja wa Mataifa ni kwa mujibu wa rekodi za zamani. Urutuki ni miongoni mwa nchi zinazolaumiwa kuchochea mapigano nchini Syria.
Katika upande mwingine zaidi ya waasi 100 wameuawa katika operesheni ya anga iliyofanywa na jeshi la serikali ya Syria dhidi ya eneo linalodhibitiwa na makundi ya waasi huko Aleppo kaskazini magharibi mwa nchi hiyo.

No comments: