Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Wito wa kufanyika maandamano ya mamilioni nchini Misri

Muungano wa kitaifa wa kuunga mkono utawala wa kisheria nchini Misri umetoa wito wa kufanyika maandamano ya mamilioni ya watu kupinga serikali ya kijeshi.
Katika taarifa yake iliyotoa leo, sambamba na kusifu muqawama wa wanafunzi wa vyuo vikuu vya Misri katika kukabiliana na serikali ya kijeshi, muungan huo umelaani mashambulizi ya kinyama ya wanajeshi watiifu kwa wafanya mapinduzi dhidi ya vyuo vikuu na kuwakandamiza waandamanaji.
Muungano huo umewataka Wamisri kujitokeza kuandamana kwa mamilioni kesho Jumanne na kusisitiza kuwa, jinai zinazofanywa na serikali ya mpito ya Cairo hazitafumbiwa macho.
 Hayo yanajiri huku serikali ya Misri ikiimarisha usalama katika Medani ya Tahriri mjini Cairo na vikosi vya usalama na magari ya jeshi yanafanya doria mjini humo. Taarifa zinasema kuwa baada ya kutolewa wito wa maandamano ya kupinga jeshi, usalama umeimarishwa kwenye majengo ya serikali na kwamba idadi kubwa ya askari na magari ya jeshi yamepelekwa kwenye maeneo mbalimbali ya mji mkuu, Cairo.

No comments: