Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, December 28, 2013

Watu wanane wauawa katika mripuko Mogadishu

Watu wanane wameuawa katika mlipuko uliotokea leo huko Mogadishu mji mkuu wa Somalia.
Watu wanane wamefariki dunia baada kuripuka bomu linaloongozwa kutokea mbali. Bomu hilo lililipuka mapema leo kwenye mgahawa mmoja huko Mogadishu mji mkuu wa Somalia.
Qadir Muhammad afisa polisi wa Somalia ameripoti kuwa wanajeshi watatu pia wameuawa katika mripuko huo na hadi sasa hakuna kundi au mtu aliyetangaza kuhusika na shambulizi hilo.
Afisa huyo wa polisi ya Somalia ameongeza kuwa wanalishuku kundi la ash-Shabab kuwa limehusika katika mripuko huo huko Mogadishu.
Kundi la wanamgambo wa ash-Shabab linadhibiti eneo kubwa la kusini na katikati mwa Somalia na limekuwa likiendesha mashambulizi dhidi ya vikosi vya serikali na wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Afrika walioko Somalia.

No comments: