Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Saturday, December 28, 2013

Waasi wa S/Kusini wadai kuudhibiti mji wa Malakal

Waasi watiifu kwa Riek Machar, makamu wa zamani wa Rais wa Sudan Kusini wamesema kuwa wameuteka mji unaozalisha mafuta kwa wingi wa Malakal baada ya mapigano ya siku tatu na vikosi vya serikali ya juba.
Moses Ruai Lat msemaji wa waasi watiifu kwa Machar amesema leo kuwa mji wote wa Malakal unadhibitiwa na vikosi vyao.
Hata hivyo Kuol Manyang Juuk, Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini amepinga madai hayo ya waasi watiifu kwa Machar akisema kuwa ni ya uwongo.
Amesema wapiganaji watiifu kwa Riek Machar wamepata kipigo na hawapo tena katika mji huo mkubwa kwa uzalishaji wa mafuta. Waziri wa Ulinzi wa Sudan Kusini amesema kuwa mji wa Malakal unadhibitiwa kikamilifu na majeshi ya serikali.
Wakatihuohuo, nchi jirani na Sudan Kusini leo zimemuunga mkono Rais Salva Kiir wa nchi hiyo baada ya siku 13 za mapigano katika nchi hiyo changa zaidi duniani. Nchi jirani na Sudan Kusini zimesema kuwa hazitakubali hatua yoyote ile ya kumuondoa madarakani Rais Kiir na serikali yake iliyochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia.
Nchi za Magharibi na zile za za Kiafrika zinahofia kuwa mapigano yanayoendelea kati ya vikosi vya serikali na waasi watiifu kwa makamu wa zamani wa Rais Salva Kiir yaani Riek Machar yanaweza kuchochea vita vya ndani vya  kikabila ambavyo vitakuwa hatari kwa nchi za eneo hilo.
Akihutubia viongozi wa kieneo katika mkutano wa dharura ulioitishwa huko Juba na Jumuiya ya Igad kujadili mgogoro wa Sudan Kusini, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya amewataka Kiir na Machar kutumia fursa iliyopo na kuanza mazungumzo ya amani.

No comments: