Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Wapinzani Libya: Tutaendele kuzuia mafuta nchini

Wapinzani wa serikali nchini Libya wametangaza kuwa wataendelea kuzingira viwanda vya uzalishaji mafuta na bandari zake, kufuatia kushindikana kufikiwa maelewano kati yao na serikali ya Tripoli. Mkuu wa gadi ya usalama ya mzingiro katika bandari za Ra's Lanuf, As Sidr na az Zaytuniyyah bwana Ibrahim Jadhran ametangaza kuwa, wapinzani hawatozifungua tena bandari hizo za mafuta kwa kuwa serikali imeshindwa kutekeleza masharti yao kabla ya kumaliza mzingiro huo.
Hii ni katika hali ambayo kiongozi mmoja wa kamisheni ya nishati katika bunge la nchi hiyo, ametangaza kuwa uzalishaji mafuta nchini Libya umepungua na kufikia kiwango cha mapipa 100 kwa siku. Kabla ya hapo Waziri Mkuu wa Libya Ali Zeidan alitangaza kuwa, kuna uwezekano wa kumalizika mzingiro wa watu wenye silaha dhidi ya bandari za kusafirishia mafuta huko mashariki mwa nchi hiyo. Ali Zeidan alisema kuwa, mzingiro huo uliodumu kwa muda mrefu sasa ulitarajiwa kumalizika ifikapo jana Jumapili na kuanza upya shughuli za usafirishaji mafuta.

No comments: