Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Sudan Kusini yazima jaribio la kupindua serikali

Rais Salva Kiir wa Sudan Kusini amesema kuwa serikali yake imezima jaribio la mapinduzi na kutangaza marufuku ya kutoka nje katika mji mkuu Juba baada ya mapigano yaliyotokea usiku wa kuamkia leo kati ya makundi hasimu ya jeshi.
Kiiri amewaambia waandishi habari mjini Juba hii leo kwamba jeshi la Sudan Kusini limefanikiwa kuzima jaribio la mapinduzi na kusisitiza kuwa, zama za mapinduzi ya kijeshi zimepitwa na wakati.

Machafuko hayo yameanza kufuatia wiki kadhaa za mivutano baada ya Rais Kiir kumuuzulu makamu wake, Rick Machar mwezi Julai. Rais wa Sudan Kusini amesema kuwa wanajeshi watiifu kwa Machar ndio waliosababisha mapigano hayo. Ripoti zinasema kuwa, Machar amekamatwa na jeshi limethibiti hali ya mambo.
Akitangaza marufuku hiyo Salva Kiir amesema kuwa, watu hawataruhusiwa kutoka nje kuanzia saa 12 jioni hadi 12 asubuhi na kuwahakikishia wananchi kwamba hali ya mambo ni shwari kwa sasa.
Salva Kiir na Rich Machar wanatoka katika makundi tofauti ya kikabila yaliyokuwa yakipigana huko nyuma.

No comments: