Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Kesi ya Mubarak yaanza kuchunguzwa Cairo, Misri

Mahakama ya mjini Cairo nchini Misri imeanza vikao vya kuchunguza faili la tuhuma zinazomkabili dikteta wa zamani wa nchi hiyo Hosni Mubarak, wanawe wawili, waziri wa mambo ya ndani wa zamani, wasaidizi wengine sita wa waziri wa mambo ya ndani na mfanyabiashara aliyetoroka nchi.
Habari zinasema kuwa, Mubarak na wanawe ambao ni Alaa na Gamal, Habib el-Adly na wasaidizi wake sita na Hussein Salim mfanyabiashara aliyekimbia wanatuhumiwa kwa kutekeleza mauaji dhidi ya waandamanaji katika mapinduzi ya wananchi ya mwaka 2011 na kupora mali za umma. Kwa mujibu wa habari SamiHafez Anan jenerali mkuu wa jeshi wa zamani nchini humo leo atatoa ushahidi katika kikao cha siri cha mahakama dhidi ya watuhumiwa hao. Siku ya Jumamosi, Mohamed Hussein Tantawi waziri wa ulinzi wa zamani wa Misri, alitoa pia ushahidi kama huo. Kikao hicho cha siku ya Jumamosi kilichofanyika kwa muda wa masaa manne, Tantawi alijibu maswali 200 kutoka bodi ya mahakama na mengine 50 kutoka kwa mawakili wa watuhumiwa.

No comments: