Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Askari wa Kizayuni auawa na jeshi la Lebanon

Askari mmoja wa utawala haramu wa Kizayuni ameuawa na vikosi vya Lebanon baada ya kuvuka mpaka na kuingia katika ardhi za nchi hiyo. Tukio hilo limetokea katika eneo la mpakani la Naqoura baada ya kuzuka mapigano kati ya askari wa Lebanon na wa utawala wa Kizayuni na kupelekea mwanajeshi mmoja wa Israel kuangamizwa. Kwa mujibu wa habari, askari mwingine mmoja wa Lebanon ameuawa katika tukio hilo.
Vikosi vya jeshi la Lebanon katika maeneo ya mpakani ya ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina vimejiweka katika hali ya hatari huku jeshi la utawala haramu wa Israel likiongeza idadi ya askari wake mpakani hapo. Tayari utawala wa Kizayuni umekiri kutokea tukio hilo. Hili ni tukio la pili kujiri ndani ya kipindi cha wiki mbili zilizopita kati ya pande mbili. Kwa mara kadhaa utalawa haramu wa Kizayuni umekuwa ukikiuka anga ya Lebanon na kuvamia ardhi za nchi hiyo mara kwa mara, huku jamii ya Kimataifa ikinyamazia kimya vitendo hivyo vya kichokozi vya Israel.

No comments: