Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, December 16, 2013

Bandar apanga njama za kuenguliwa Salman

Duru za habari nchini Saudia zinefichua kuwa, Bandar bin Sultan bin Abdulaziz Al Saud Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Saudi Arabia anapanga njama za kumpindua  Salman bin Abdulaziz Al Saud mrithi wa kiti cha ufalme nchini humo. Habari zinaeleza kuwa, hivi karibuni Bandar alieneza uvumi kwamba, mrithi huyo wa kiti cha mfalme hawezi kutekeleza majukumu yake kutokana na kuelemewa na ugonjwa. Ripoti hizo zimeongeza kuwa, Mkuu huyo wa Shirika la Ujasusi la Saudi Arabia ameanza mchakato wa kufanya mazungumzo na mfalme wa Saudia kwa lengo la kutaka achaguliwe mwana mfalme Muqrin bin Abdulaziz Al Saud au mtu mwingine ambaye ataweza kutekeleza majukumu yake vizuri.
Nivyema kuashiria hapa kwamba Muqrin alikuwa akishikilia nafasi ya Mkuu wa Shirika la Ujasusi la Saudi Arabia kabla ya Bandar hajachaguliwa katika nafasi hiyo. kwa mujibu wa habari banda anafanya njama hizo kwa lengo la kupanua satwa yake ya uongozi nchini Saudia.

No comments: