Tume ya Kuajiri Walimu nchini Kenya (TSC) imeanzisha mikakati ya kuajiri
walimu wapya watakaochukua nafasi za wale wanaogoma. Kwa mujibu wa tume
hiyo, walimu watakaopoteza nafasi zao za kazi ni wale waliokosa kurudi
kazini kuambatana na agizo la mahakama lililotolewa Julai 1, na
waliokataa kutii amri ya serikali iliyotolewa Jumatatu iliyopita.
Agizo
la serikali lililotolewa na Waziri wa Elimu, Prof. Jacob Kaimenyi,
lilisema walimu ambao wangekosa kurudi kazini Jumanne ya jana
wangechukuliwa kama waliokwepa kazi na kuadhibiwa. Prof Kaimenyi alikuwa
amesema TSC ina mamlaka ya kuchukua hatua dhidi ya walimu waliokosa
kurudi kazini, kwa kuwa sheria inaruhusu mwajiri kumwadhibu muajiriwa
wake anapokosa kuhudumu inavyostahili. Tayari TSC imewataka watu
waliohitimu katika taaluma ya uwalimu watume maombi ya kazi. Hata
hivyo, mwenyekiti wa chama cha kitaifa cha walimu nchini Kenya KNUT, Bw.
Wilson Sossion, amepuuzilia mbali harakati za TSC na kuitaka serikali
kukoma kuwatisha walimu na badala yake iwalipe marupurupu yao. Mgomo wa
walimu katika shule za umma kote nchini Kenya umeingia wiki ya 3 sasa
huku zikiwa zimesalia wiki chache kabla ya muhula wa pili kumalizika.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment