Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Misri yaitaka Uturuki kukoma kuingilia mambo yake

Serikali mpya ya Misri imeitaka Uturuki kukoma mara moja kuingilia mambo yake ya ndani. Hii ni baada ya Waziri Mkuu wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan kusema mara kadhaa kwamba nchi yake bado inamtambua Mohammad Mursi kuwa rais halali wa Misri. Jumapili iliyopita, Erdogan aliiambia kanali moja ya televisheni ya Uturuki kwamba Ankara haiwezi kuunga mkono mapinduzi ya kijeshi yaliyofanyika Misri majuma mawili yaliyopita.
Wizara ya Mambo ya Nje ya Misri imetoa taarifa na kuyataja matamshi hayo ya Erdogan kuwa uingiliaji wa mambo ya ndani ya nchi hiyo na kumtaka kiongozi huyo kuacha kabisa tabia hiyo. Dkt. Muhammad Mursi alikuwa muitifaki mkubwa wa Waziri Mkuu wa Uturuki hususan katika kadhia ya Syria na kuondolewa kwake madarakani kumetoa pigo kubwa kwa kiongozi huyo na serikali ya Ankara kwa ujumla.

No comments: