Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 15, 2013

Wamarekani weusi wapinga hukumu ya mahakama

Jamii ya watu weusi nchini Marekani imelaani hukumu iliyotolewa na jopo la majaji kuhusu kesi ya mauaji dhidi ya George Zimmerman. Zimmerman alikuwa anakabiliwa na mashtaka ya kumuua Trayvon Martin, Mmarekani mweusi mwenye umri wa miaka 17.  Jopo hilo la majaji limetoa uamuzi huo leo alfajiri kwa saa za hapa Tehran ambapo limesema Zimmerman hana hatia na kwamba uchunguzi unaonyesha hakuhusika na mauaji hayo.
Wazazi wa Travyon wamesema wanamuachia Mungu hayo yote na kusisitiza kwamba hawajaridhishwa na uamuzi huo. Wamarekani weusi wamesema uamuzi wa jopo hilo unairudisha nchi katika zama za ubaguzi wa rangi na wameitaka mahakama ya kilele ya Marekani kuingilia kati suala hilo. Maandamano yameripotiwa katika maeneo kadhaa ya Francisco huku waandamanaji wakibeba mabango yenye jumbe za kulaani uamuzi huo. Baadhi ya mabango yalikuwa na maandishi yanayosema: "Mfumo mzima ni wa kibaguzi" "Wananchi tunasema Zimmerman ni muuaji"  

No comments: