Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

UN na EU zaahidi kuwasaidia wahanga wa CAR

Maafisa wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya wameahidi kuwasaidia wahanga wa mgogoro uliosahaulika huko Jamhuri ya Afrika ya Kati. Valerie Amos Naibu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na Masuala ya Kibinadamu na ambaye pia ni Mratibu wa Misaada ya Dharura wa Umoja huo na Kristalina Georgieva Kamishna wa Umoja wa Ulaya anayehusika na Ushirikiano wa Kimataifa ambao wako katika ziara ya siku mbili huko Jamhuri ya Afrika ya Kati jana walitembelea mji wa Kaga Bandoro umbali wa kilomita 350 kaskazini mwa Bangui mji mkuu wa nchi hiyo.
Wakiwa ziarani Kaga Bandoro, maafisa hao wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Ulaya walizungumza na wenyeji na maafisa wa mji huo na kuwaeleza kuwa hali inayowakabili sasa haitakuwa tena mgogoro uliosahaulika. Wamesema wako ziarani mjini humo ili kujua matatizo yao na kuifanya jamii ya kimataifa izingatie mgogoro unaowakabili. Shule, ofisi za serikali na majego ya Umoja wa Mataifa katika mji huo yamekabiliwa na vitendo vya uporaji mara kadhaa tangu waasi wa Muungano wa Seleka wachukue madaraka mwezi Machi mwaka huu.  Mashambulizi ya mara kwa mara ya makundi yenye silaha katika mji wa Kago Bandoro huko Jamhuri ya Afrika ya Kati yamewapelekea wakazi wengi wa mji huo kuishi katika misitu ya jirani na kuishi kwa kutegemea mizizi pamoja na majani ya miti ya mihogo. 

No comments: