Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Sunday, July 14, 2013

Wabahraini: Mateso ya wafungwa yachunguzwe

Wananchi wa Bahrain wamefanya maandamano na kusisitiza kuundwa kamati zisizoegemea upande wowote ili kuchunguza mateso wanayofanyiwa wafungwa wa kisiasa nchini humo. Wananchi wa Bahrain jana usiku walifanya maandamano makubwa huko Manama mji mkuu wa nchi hiyo na kutaka kuhukumiwa wale wote wanaohusika katika uwanja huo.
Katika maandamano hayo, wananchi wa Bahrain walipiga nara wakisisitiza juu ya udharura wa kuachiwa huru haraka iwezekanavyo wafungwa wote wa kisiasa na kukomeshwa mateso dhidi yao katika jela za utawala wa Aal Khalifa. Naye Sheikh Ali Suleiman Katibu Mkuu wa Taasisi ya Kitaifa ya al Wifaq amesisitiza mwishoni mwa maandamano hayo juu ya udharura wa kukomeshwa ukiukwaji wa haki za binadamu huko Bahrain na kueleza kuwa matabaka yote ya wananchi nchini yanataka kuundwa serikali ya kiraia.  Hii ni kwa sababu wamechoshwa na ubaguzi na ukandamizaji wa utawala wa kifalme wa Aal Khalifa.

No comments: