Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, January 24, 2013

Magaidi wanaoungwa mkono na Saudia wakamatwa Iraq

Vikosi vya Usalama Iraq vimewatia mbaroni magaidi 250 wenye itikadi ya pote la Kiwahhabi na ambao wanapata himaya ya utawala wa Saudi Arabia.
Magaidi hao waliokamatwa katika eneo la Euphrates ya Kati walikuwa wakipanga njama ya kutekeleza oparesheni katika miji ya Iraq ya Karbala, Najaf na ad-Diwaniya.
Kwa mujibu maafisa wa usalama wa Iraq, mkuu wa shirika la ujasusi la Saudia Bandar bin Sultan ametoa dola milioni 250 kwa ajili ya kufadhili oparesheni za kigaidi kote Iraq.

Aidha duru za usalama za Iraq zinasema Bandar bin Sultan amemkabidhi makamu wa rais mtoro wa Iraq Tariq al Hashemi jukumu la kutekeleza oparesheni za kigaidi nchini humo. Magaidi waliokamatwa wamekiri kutekeleza mauaji ya malaki ya Wairaqi wasio na hatia.

No comments: