Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 15, 2013

Mapigano makali kati ya jeshi la Kongo na Mai Mai

Mapigano makali yamejiri kati ya vikosi vya jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na kundi la wanamgambo huko mashariki mwa nchi hiyo. Wakazi wa eneo la Nyamilima la mashariki mwa mkoa wa Kivu Kusini wamesema kuwa, vikosi vya jeshi la Kongo vimeshiriki katika mapigano makali na watu hao waliokuwa na silaha waliowataja kuwa wanamgambo wa Mai Mai.
Mapigano hayo yalitokea jana Jumamosi huko mashariki mwa Kongo. Wanajeshi wa Kongo waliamua kuwashambulia wanamgambo wa Mai Mai baada ya kutiwa mbaroni kiongozi wao na baada ya jeshi la Kongo kuchoshwa na vitisho vya mara kwa mara vya wanamgambo hao. Jeshi la Kongo limesema limefanikiwa kuwafukuza wanamgambo wa Mai Mai huko Nyamilima na kwamba oparesheni zao dhidi ya wanamgambo hao zitaendelea.

No comments: