Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 18, 2013

Wamarekani waendelea kupinga ubaguzi

Polisi ya Marekani imeendelea kuwatia nguvuni waandamanaji wanaopinga hukumu ya mahakama ya nchi hiyo iliyomuachia huru askari aliyemuua Mmarekani kijana mwenye asili ya Afrika kwa kumpiga risasi bila ya hatia yoyote. Ripota wa Press tv amesema Wamarekani waliendelea kuandamana jana katika miji ya California na Los Angeles
wakipinga uamuzi wa mahakama ya Florida wa kumuondoa hatiani askari wa zamu George Zimmerman aliyemuua kijana Mmarekani-Mwafrika ambaye hakuwa na silaha yoyote wakati anauawa.
Mjini Washington pia wapinzani wa hukumu ya mahakama hiyo walikusanyika kwa siku ya pili mfululizo mbele ya Ikulu ya White House kuonesha hasira zao dhidi ya uamuzi huo uliotambuliwa na wengi kuwa umetolewa kwa misingi ya kibaguzi.
Maandamano na ghasia kubwa za kupinga ubaguzi unaofanywa na vyombo vya usalama na mahakama za Marekani dhidi ya Wamarekani wenye asili ya Afrika pia zimeshuhudiwa katika miji mbalimbali ya Marekani.
Machafuko hayo yalianza Jumamosi iliyopita baada ya mahakama moja ya Florida kumuondoa hatiani mlinzi mzungu Zimmerman aliyemuua kijana Mmarekani-Mwafrika Trayvon Martin ambaye hakuwa na silaha.
Wanaharakati wa haki za kiraia wanapanga kuitisha maandamano makubwa katika miji mia moja ya Marekani Jumamosi ijayo kupinga ubaguzi unaowalenga Wamarekani wenye asili ya Afrika.

No comments: