Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 18, 2013

Ashton: Mursi aachiwe huru

Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya Catherine Ashton ameutaka utawala wa sasa wa Misri kumuachia huru rais aliyeondolewa madarakani wa nchi hiyo Muhammad Mursi na wanasiasa wengine wanaoshikiliwa na jeshi la nchi hiyo.
Ashton alitoa wito huo jana mjini Cairo katika mazungumzo yake na viongozi wapya wa Misri akiwemo Rais wa muda wa nchi hiyo Adly Mansour.

Catherine Ashton amewaambia waandishi habari kwamba, amewataka viongozi wa sasa wa Cairo kumwachia huru Mursi na wanasiasa wengine wa Harakati ya Ikhwanul Muslimin kama hawakabiliwi na tuhuma za aina yoyote. Amesema alitaka kukutana na Mursi anayeshikiliwa na jeshi mahala pasipojulikana, lakini hakufanikiwa.
Wakati huo huo maelfu ya wananchi wa Misri wameendelea kufanya maandamano katika miji mbalimbali ya nchi hiyo wakitaka kurejeshwa madarakani Muhammad Mursi.
 

No comments: