Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 12, 2013

Wafuasi 84 wa Gbagbo wapandishwa kizimbani

Mahakama moja ya mjini Abidjan imesikiliza kesi ya wapambe 84 wa karibu wa rais wa zamani wa nchi hiyo Laurent Gbagbo. Miongoni mwa watuhumiwa hao ambao hadi sasa wanaendelea kushikiliwa katika jela za Kodivaa ni pamoja na Simone Gbagbo, mke wa rais huyo wa zamani na Michel Gbagbo mtoto wa kiume wa Gbagbo.
Watu hao wanatuhumiwa kutenda jinai za makusudi za kuhujumu uchumi, jinai za kivita, kuzusha machafuko katika jamii na kushirikiana na magenge ya watu wenye silaha kwa lengo la kuiangusha serikali ya hivi sasa nchini humo. Aidha mwendesha mashtaka amewasomea mashataka watu wengine wanane kwa kutenda jinai ya mauaji ya kizazi. Weledi wengi wa masuala ya kisiasa wameitaja hatua hiyo iliyochukuliwa na mahakama kuwa haikutazamiwa.

No comments: