Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 12, 2013

Venezuela: Hatujapata majibu kutoka kwa Snowden

Waziri wa Mambo ya Nje wa Venezuela, ElíasJosé Jaua, amesema kuwa, hadi sasa afisa wa zamani wa Shirika la kijasusi la Marekani CIA, Bw. Edward Snowden hajatoa majibu juu ya pendekezo la nchi hiyo la kumpa hifadhi. Elíasamesema, serikali ya Caracas haina mawasiliano na afisa huyo wa kijasusi wa Marekani.
Waziri huyo wa Mashauri ya Kigeni wa Venezuela ameyasema hayo alipokuwa akijibu swali lililotaka kujuwa kama serikali yake imepata majibu kutoka kwa Snowden baada ya Rais Nicolás Maduro wa nchi hiyo kutangaza kumpatia hifadhi afisa huyo wa zamani wa CIA. Ijumaa iliyopita rais wa Venezuela alitoa pendekezo la kumpatia hifadhi ya urafiki Snowden. Venezuela ilichukua hatua hiyo kwa kile ilichosema kuwa ni kuzuia kuhukumiwa afisa huyo kinyume cha sheria katika vyombo vya sheria vya Marekani.

No comments: