Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 12, 2013

UN yasisitiza kuongezwa vikosi vyake S/Kusini

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limesisitizia udharura wa kuongezwa idadi ya vikosi vyake nchini Sudan Kusini.
Baraza hilo limefikia uamuzi huo katika kikao maalumu kilichofanyika kwa madhumuni ya kurefushwa kazi za askari wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa katika nchi kadhaa duniani ikiwemo Sudan Kusini na kusisitizwa juu ya udharura wa kutumwa vikosi zaidi katika maeneo ya mapigano, likiwemo eneo la Jonglei huko Sudan Kusini.

Mapigano katika jimbo hilo kati ya jeshi la Sudan Kusini na makundi ya wabeba silaha, yamepelekea makumi ya maelfu ya raia kuwa wakimbizi na wengine kuuawa wakiwemo askari watano wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa.

No comments: