Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 18, 2013

UN yatafakari kusitisha msaada kwa jeshi la DRC

Umoja wa Mataifa umesema unafikiria suala la kusitisha msaada kwa Jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (FARDC) baada ya kubainika kwamba baadhi ya wanajeshi wa serikali wamekuwa wakiivunjia heshima miili ya waasi wa M23 waliouawa vitani na kuwatesa wafungwa.
Akizungumza jana Jumatano, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban-Ki-moon alielezea wasi wasi wake kuhusu
vitendo hivyo vya askari wa Kongo katika kipindi hiki cha kushadidi mapigano mashariki mwa nchi hiyo.
Jeshi la Kongo limesema litachunguza tuhuma hizo na kuwachukulia hatua za kisheria wahusika. Jeshi la Kongo linaendeleza mashambulizi dhidi ya ngome za waasi wa M23 karibu na mji wa Goma na kupelekea mamia ya wanakijiji kukimbia makaazi yao.  Katika taarifa jeshi hilo la limeeleza kuwa, limeanza kushambulia kwa makombora eneo la Kibati lililoko umbali wa kilomita 15 kaskazini mwa Goma, makao makuu ya jimbo la Kivu Kaskazini.
Waasi wa M23 walianza kuchukua udhibiti wa baadhi ya maeneo ya mashariki mwa Kongo mwaka jana kwa madai kuwa serikali ya Kinshasa haijatekeleza makubaliano ya amani ya mwaka 2009.

No comments: