Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Ubaguzi wasababisha Machafuko Marekani

Watu wenye hasira wameandamana kote nchini Marekani kulaani uamuzi wa mahakama moja nchini humo wa kumuondoa hatiani George Zimmerman aliyemuua kijana Mmarekani-Mwafrika.
Maandamano makubwa yameripotiwa kufanyika huko Oakland, California, Los Angeles, New York, Boston na San Francisco.
Machafuko Marekani yalianza Jumamosi baada ya mahakama moja ya Florida kumuondoa hatiani mlinzi Zimmerman ambaye alimuua kijana Mmarekani-Mwafrika Trayvon Martin ambaye hakuwa na silaha.
Waandamanaji walibeba mabango yaliyokuwa na maandishi kama vile 'Tunataka Uadilifu' na  'Komesheni Ubaguzi'.
Duru zinaarifu kuwa idadi kubwa ya watu wametiwa mbaroni huku polisi wakionekana kutumia mabavu dhidi ya waandamanaji. Wamarekani wenye hasira wamekaidi ombi la rais Barack Obama ambaye amewataka watulie na waheshimu uamuzi wa mahakamana.

No comments: