Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Djotodia: Rais Bozize anaweza kurejea CAR

Rais Michel Djotodia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati amesema, rais wa zamani wa nchi hiyo aliyeondolewa madarakani katika mapinduzi ya mwezi Machi mwaka huu sasa anaweza kurejea nchini humo. Akiwa ziarani nchini Benin, Rais wa Jamhuri ya Afrika ya Kati amesema kuwa, Francois Bozize ni raia wa Jamhuri ya Afrika ya Kati kwa hivyo anaweza kurejea nchini kwake na kwamba wao hawapingi jambo hilo.
Mwezi Mei mwaka huu viongozi wa Jamhuri ya Afrika ya Kati walitoa waranti wa kutiwa mbaroni Bozize wakimtuhumu kutenda jinai dhidi ya binadamu na kuchochea mauaji ya kimbari nchini humo. Hata hivyo rais wa hivi sasa wa Jamhuri ya Afrika ya Kati hakusema iwapo Francois Bozize atatiwa nguvuni atakaporejea nchini humo au la. Baada ya kupinduliwa, Bozize alikimbilia nchini Cameroon, lakini sasa hajulikani aliko.

No comments: