Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Rais Bouteflika wa Algeria arejea nyumbani

Duru za habari kutoka Ufaransa zinaarifu kuwa, Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria amerejea nchini kwake baada ya kupata matibabu nchini Ufaransa. Habari zinasema kuwa, Rais Bouteflika ameondoka nchini Ufaransa majira ya adhuhuri ya leo kuelekea nchini kwake. Rais huyo mwenye umri wa miaka 76 alipelekwa nchini Ufaransa baada ya kukumbwa na ugonjwa wa kiharusi mwishoni wa mwezi Februari ambapo awali alilazwa katika hospitali ya kijeshi ya Valde Grace na kupelekwa katika hospitali nyingine ya mjini Paris, Ufaransa.
Kukosekana kwake kisiasa nchini Algeria, kuliibua maswali mengi hasa kuhusiana na nafasi ya uraisi nchini humo. Hali hiyo ilivifanya vyama na makundi ya kisiasa yanayoipinga serikali inayoongozwa na Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria, vilitaka kufanyika uchaguzi wa kabla ya wakati kwa mujibu wa katiba ya nchi hiyo kutokana na kuugua rais huyo. Hii ni katika hali ambayo hivi karibuni Rais huyo alitoa msamaha kwa maelfu ya wafungwa wa nchi yake, kwa mnasaba wa kuwadia sherehe za kumbukumbu za uhuru wa nchi hiyo.

No comments: