Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 19, 2013

Sudan: Wamisri watatue matatizo yao wenyewe

Kwa mara nyingine serikali ya Sudan imesisitiza kuwa, taifa la Misri linaweza kumaliza lenyewe mgogoro ulioikumba nchi hiyo hivi sasa. Hayo yamesemwa na Naibu Spika wa bunge la Sudan Samiya Ahmad Muhammad alipokuwa akiongea na waandishi wa habari katika ofisi za bunge na kufafanua kuwa, taifa la Misri linaweza lenyewe kumaliza mgogoro wa nchi hiyo ili kwa mara nyingine taifa hilo muhimu liweze
kutoa mchango wake chanya katika ulimwengu wa Kiarabu na Kiislamu na duniani kiujumla. Aidha ameashiria kwamba, matatizo ya Misri ni ya ndani na kusisitiza kuwa, serikali ya Khartoum huwa haiingilii masuala ya ndani ya nchi yoyote duniani. Kwa upande mwingine Naibu Spika wa Bunge la Sudan amesisitizia kuwepo uhusiano mwema baina ya nchi yake na mataifa mbalimbali ya dunia. Hii ni katika hali hali ambayo mamia ya Watunisia kwa mara nyingine leo wamefanya maandamano kumuunga mkono rais aliyeenguliwa madarakani Muhammad Mursi wa Misri. Waandamanaji hao waliokuwa na picha za Mursi, walitoa nara za kulaani hatua ya jeshi la Misri ya kuingilia masuala ya siasa nchini humo.

No comments: