Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 19, 2013

ICC yapata pigo katika kesi za viongozi wa Kenya

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Jinai ICC, Bi. Fatou Bensouda, ameondoa mashahidi watatu kwenye kesi ya jinai dhidi ya binadamu inayomkabili Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya. Bensouda amesema mashahidi wawili wamesisitiza kwamba hawawezi kuendelea kuwa mashahidi kwenye kesi hiyo kutokana na kuhofia usalama wao.
Amesema pia kuwa, ametathmini ushahidi wa shahidi mwengine na ameona hauna umuhimu mkubwa na kwa mantiki hiyo ameamua kumuondoa. Itakumbukwa kuwa mahakama hiyo ya ICC majuma kadhaa yaliyopita iliamua kwamba, Makamu wa Rais wa Kenya, William Ruto atahudhuria tu vikao muhimu vya kesi yake mjini Hague na kisha kushiriki kwenye vikao vya kawaida kwa njia ya video. Wachambuzi wa masuala ya kisheria wanasema hatua hiyo ina maana kwamba kesi dhidi ya Rais Kenyatta na Makamu wake zinaendelea kuwa dhaifu na huenda wakafutiwa mashtaka iwapo matukio kama hayo yataendelea kushuhudiwa.

No comments: