Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, July 19, 2013

Araqchi akaribisha nia njema ya Uingereza kwa Iran

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Abbas Araqchi, amekaribisha matamshi ya Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza, William Hague ambaye amesema nchi yake iko tayari kuimarisha uhusiano na Iran hatua kwa hatua. Bw. Araqchi amesema Jamhuri ya Kiislamu ya Iran iko tayari kuimarisha uhusiano na nchi zote za Ulaya ikiwemo
Uingereza ilimradi uhusiano huo uwe wa kimantiki na unaoheshimu maslahi ya pande mbili. Kauli ya Msemaji wa Wizara ya Mambo ya nje ya Iran inakwenda sanjari na yale ya rais mteule, Dk Hassan Rohani ambaye amekariri mara kadhaa kwamba sera za nje za serikali yake zitalenga kuimarisha uhusiano na nchi zote duniani. Rohani amekuwa akisisitiza kwamba dunia inahitaji mchango wa kila nchi ili mambo yawe shwari. Hata hivyo, Sheikh Hassan Rohani amesema uhusiano wowote ule lazima ujengeke juu ya misingi ya uadilifu na kuheshimiana.

No comments: