Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Russia: 5+1 ina hamu ya kuzungumza na Iran

Wizara ya Mambo ya Nje ya Russia imesema kuwa jamii ya kimataifa ina hamu kubwa ya kufanya mazungumzo na serikali ijayo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuhusu kadhia yake ya nyuklia. Taarifa hiyo imesema kwamba, hapo jana wanadiplomasia wa Marekani, Uingereza, Ufaransa na Uchina walikubaliana kwa kwauli moja kuwa, duru mpya ya mazungumzo na Iran inapaswa kuanza punde tu serikali mpya itakapoanza kazi baada ya kuapishwa rais mteule, Dkt. Hassan Rohani.
Kauli kama hiyo pia ilitolewa na Bi. Catherine Ashton, Mkuu wa Sera za Nje wa Umoja wa Ulaya hapo jana ambapo alisema kundi la 5+1 linatarajia kuanza mazungumzo na Iran ili kutatua suitafahamu iliyoko kuhusu kadhia yake ya nyuklia. Ashton amesema kundi hilo linalojumuisha nchi 5 wanachama wa kudumu wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa pamoja na Ujerumani lina matumaini kwamba litaweza kufikia makubaliano muhimu na serikali ijayo ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.

No comments: