Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

UN: Eritrea inatumia wababe wa kivita nchini Somalia

Kamati ya wataalamu wa Umoja wa Mataifa inayochunguza utekelezwaji wa vikwazo vya Baraza la Usalama la umoja huo katika nchi za Somalia na Eritrea imedai kwamba Asmara imekuwa ikutumia wababe wa kivita ili kuhujumu amani nchini Somalia. Kamati hiyo imetaja baadhi ya wababe wa kivita wa Somalia ambao hupokea fedha na taarifa za kiintelijensia kutoka Eritrea na kusema kuwa, fedha na taarifa hizo hutumiwa na makundi yenye misimamo mikali kutekeleza mashambulizi nchini Somalia.
Wataalamu wa UN pia wamesisitiza kwamba Eritrea bado ina uhusiano wa moja kwa moja na kundi la kigaidi la al-Shabab. Eritrea kwa upande wake imekanusha madai hayo na kusema yanachochewa kisiasa na nchi jirani ya Ethiopia. Asmara imesisitiza kuwa haina uhusiano wowote na makundi ya kigaidi kokote duniani na kwamba vikwazo vya Umoja wa Mataifa dhidi yake si halali na imetaka vikwazo hivyo kuondolewa.

No comments: