Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Rais Bouteflika, aachia huru maelfu ya wafungwa

Rais Abdelaziz Bouteflika wa Algeria, ametoa msamaha kwa maelfu ya wafungwa kwa mnasaba wa kuwadia sherehe za kumbukumbu za uhuru wa nchi hiyo. Rais Bouteflika ambaye bado anaendelea kupata matibabu nchini Ufaransa, alitoa msamaha huo hapo jana kwa mnasaba wa kumbukumbu za miaka 51 ya uhuru wa taifa hilo. Kwa mujibu wa ripoti hiyo, wafungwa waliopata msamaha ni 5, 600 ambao walikuwa ima tayari wamekwishatumikia kifungo au ndio kwanza walikuwa wamehukumiwa.
Hata hivyo wafungwa ambao wanahusika katika uvunjifu wa amani na maridhiano ya kitaifa nchini au kuhusika katika jinai maalumu ikiwemo vitendo vya kigaidi, hawatoachiliwa huru. Zimepita siku 70 huku Rais Abdelaziz Bouteflika akiendelea kusalia Ufaransa kwa matibabu ya mshituko wa ubongo. Hivi karibuni vyama na makundi ya kisiasa yanayopinga serikali ya Algeria vilitaka kufanyika uchaguzi wa kabla ya wakati kwa mujibu wa katiba kutokana na kuugua rais huyo.

No comments: