Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 8, 2013

Sudan: Tutaendelea kusafirisha mafuta ya S/Kusini

Serikali ya Sudan imetangaza kuwa, haitotekeleza vitisho ilivyokuwa imevitoa hapo kabla dhidi ya Sudan Kusini, juu ya kufunga mabomba ya usafirishaji mafuta ya nchi hiyo katika ardhi yake. Hayo yamesemwa na Rabiu Abdul-Aatwi mmoja wa viongozi wa Chama cha Kongresi ya Kitaifa cha Sudan na kuongeza kuwa, hatua hiyo imekuja baada ya makubaliano yaliyofikiwa katika kikao cha wiki iliyopita kati ya Makamu wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar na Ali Othman Taha, Makamu wa Rais wa Sudan.
Mwanzoni mwa mwezi Juni mwaka huu, serikali ya Khartoum ilitishia kusimamisha usafirishaji wa mafuta ya Sudan Kusini na kutoa fursa ya siku 60 kabla ya kuanza hatua hiyo. Hatua hiyo ilichukuliwa baada ya Rais Omar Hassan Ahmad Al-Bashir wa Sudan kuituhumu Sudan Kusini kwa kuwaunga mkono waasi dhidi ya nchi yake. Hata hivyo serikali ya Juba ilipinga vikali tuhuma hizo na kuzitaja kuwa, zisizo na ukweli wowote ule.

No comments: