Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Rais Adly Mansour aapisha serikali yake

Rais Adly Manosur wa serikali ya mpito ya Misri ameapisha serikali ya kwanza ya nchi hiyo tangu jeshi limpindue rais wa zamani wa nchi hiyo Mohamed Morsi wiki mbili zilizopita. Hazem el Beblawi, mchumi mwenye fikra za kiliberali jana jioni alikula kiapo mbele ya Rais Adly Mansour kuongoza serikali ya mpito ya Misri akiwa Waziri Mkuu Mpya.
Aidha Abdul Fatah as Sisi, mkuu wa jeshi la Misri ambaye aliongoza mapinduzi dhidi ya Morsi amekula kiapo cha kuwa Makamu wa Kwanza wa Waziri Mkuu huku akiendelea kushikilia wadhifa wake wa Waziri wa Ulinzi. Naye Nabil Fahmy ambaye alikuwa balozi wa Misri mjini Washington kuanzia mwaka 1999 hadi 2008 ameteuliwa kuwa Waziri wa Mambo ya Nje huku Mohammed Ibrahim aliyekuwa Waziri wa Mambo ya Ndani wa serikali ya Morsi akisalia katika wadhifa huo. Baraza jipya la mawaziri la serikali ya mpito ya Misri limewajumuisha pia wanawake watatu akiwemo Waziri wa Afya Maha ar Rabat. Wakati huo huo harakati ya Ikhwanul Muslimin ya Misri imepinga baraza hilo jipya la mawaziri ikisema kuwa serikali hiyo si halali.

No comments: