Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Monday, July 15, 2013

Serikali ya Sudan yaomba msaada wa IMF

Waziri wa Fedha wa Sudan ameuomba Mfuko wa Fedha wa Kimataifa (IMF) kuisaidia nchi yake. Abdurrahman Sarar, Waziri wa Fedha wa Sudan amesema, chanzo kikuu cha matatizo ya hivi sasa ya kiuchumi wa Sudan ni vikwazo na madeni ya kigeni kwa nchi hiyo. Abdurrahman Sarar ameiomba IMF kuisaidia Sudan kuinua uchumi wake.
Waziri wa Fedha wa Sudan amesema, uchumi wa nchi hiyo kwa asilimia mia moja unategemea mapato ya kigeni. Abdurrahman Sarar ameashiria pia safari za ujumbe wa IMF huko Khartoum na kueleza kuwa, pande mbili za IMF na Sudan zimefikia makubaliano mbalimbali ili kuweza kutataua matatizo ya kiuchumi ya Sudan. Waziri huyo wa Fedha wa Sudan amesema, uchumi wa nchi hiyo umeboreka kwa kiwango fulani mwaka huu ikilinganishwa na mwaka uliopita.

No comments: