Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, June 19, 2013

UN: Idadi ya wakimbizi yaongezeka duniani

Umoja wa mataifa umesema kuwa, watu milioni 7.6 walifanywa kuwa wakimbizi mwaka 2012 huku idadi kamili ya wakimbizi wote duniani ikiwa juu zaidi kuliko ilivyokuwa mwaka 1994. Takwimu mpya zilizotolewa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalowashughulikia wakimbizi (UNHCR) zimebaini kuwa idadi ya watu wanaolazimishwa kutoroka makaazi yao imepanda kwa kiasi kikubwa tangu mizozo ya Rwanda na iliyokuwa Yugoslavia.
Shirika hilo linasema kuwa mwaka jana pekee watu millioni 8 walikuwa wakimbizi huku mgogoro unaondelea Syria ukichangia pakubwa kupanda kwa idadi hiyo. UNHCR imeongeza kuwa, nusu ya wakimbizi millioni 45 ulimwenguni wanatoka mataifa ya Afghanistan, Iraq, Syria, Sudan na Somalia. Shirika hilo la wakimbizi linasema kuongezeka kwa idadi ya wakimbizi ni dhihirisho kuwa jamii ya kimataifa imeshindwa kusuluhisha mizozo iliopo na hata kuzuia mingine kujitokeza.

No comments: