Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, May 20, 2014

Mazungumzo ya Taliban na Islamabad mashakani

Kiongozi wa kundi la Taliban nchini Pakistan ametangaza vita dhidi ya serikali na hivyo kuyaweka mazungumzo ya pande mbili hizo katika hali ya hathati. Mkuu wa kundi linalojiita Tehreek-e-Taliban Pakistan (TTP) amesema wapiganaji wake wataendeleza mapambano dhidi ya serikali hadi pale sheria za Kiislamu zitakapotawala nchi hiyo. Mullah Fazlullah amesema wanaotaka kufanya mazungumzo na serikali wajue chuma chao ki motoni. TTP ni kundi lenye misimamo mikali miongoni mwa mapote kadhaa ya Taliban nchini Pakistan.
Wanamgambo wenye misimamo ya wastani wamekuwa wakifanya mazungumzo na serikali ya Islamabad kwa lengo la kufikia makubaliano yatakayohitimisha vita vya miaka kadhaa kati ya pande mbili hizo. Hata hivyo tangazo la vita la TTP dhidi ya serikali huenda likaathiri mazungumzo hayo na kuilazimisha serikali kutafuta mbinu mbadala za kukabiliana na hujuma za Taliban.   

No comments: