Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Rwanda yaituhumu Congo na askari wa kofia bluu

Rwanda imelituhumu jeshi la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na vikosi vya Umoja wa Mataifa kwamba, vimeshambulia kwa mabomu vijiji kadhaa vya Rwanda. Taarifa ya Rwanda imesema kuwa, jeshi la Congo na kikosi cha askari wa kofia ya bluu wa Umoja wa Mataifa  wamevishambulia kwa mabomu vijiji viwili vya Rwanda jirani na maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Kanali Joseph Nzabamwita msemaji wa jeshi la Rwanda amewaambia waandishi wa habari kwamba, vijiji vilivyoshambuliwa ni vya Kagashi na Gasiza vilivyoko kilomita takribani kumi na mbili kaskazini mwa Rubavu. Ameongeza kuwa, maeneo yaliyoshambuliwa yako chini ya udhibiti wa vikosi vya Congo DRC na vile vya Umoja wa Mataifa. Rwanda na Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo kila moja imekuwa ikimtuhumu mwenzake kwamba, anayaunga mkono makundi ya waasi.

No comments: