Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 18, 2013

AU yaomba ushirikiano katika kupambana na ugaidi

Umoja wa Afrika (AU) umetoa wito wa kuzidishwa juhudi za kung'oa mizizi ya ugaidi nchini Somalia.
Mjumbe malumu wa Umoja wa Afrika katika masuala ya Somalia Mahamat Saleh Annadif amesisitiza kuwa nchi za Kiafika zinapaswa kushirikiana zaidi katika kupambana na ugaidi nchini Somalia.

Amesema ugaidi haujui mipaka ya nchi na ametoa wito wa kuwepo ushirikiano na mikakati mikubwa zaidi ya kupambana nao.
Wapiganaji wa kundi la al Shabaab wanaodhibiti baadhi ya maeneo ya Somalia wamekuwa wakijitangaza kuwa na uhusiano la kundi la kigaidi la al Qaida. Wapiganaji wa kundi hilo wamekuwa wakishambulia maeneo mbalimbali ya Somalia na hata katika nchi jirani na kuua watu wasio na hatia kwa kutumia visingizio mbalimbali.

No comments: