Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Thursday, July 18, 2013

Rais Ahmadinejad: Kura za wananchi ziheshimiwa

Rais Mahmoumd Ahmadinejad wa Iran amesema kuwa watu wote wanapaswa kuheshimu kura na matashi ya wananchi.
Rais Ahmadinejad ambaye alikuwa akihutubia hadhara ya mabalozi na wawakilishi wa nchi za Kiislamu mjini Tehran ameashiria hali ya mambo katika baadhi ya nchi za Waislamu na akesema, njia pekee ya kupatikana haki za kimsingi ni maelewano na udugu.
Amesema uadilifu, uhuru na utukufu haviwezi kupatikana kwa njia ya mauaji, mapigano na vita vinavyoua watu na kuharibu uchumi, mbali na kupandikiza vinyongo katika roho za watu. Amesema viongozi wanaotwaa madaraka kwa njia ya vita wanajipalilia njia ya kuondolewa madarakani kwa njia hiyo hiyo.
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu mesema, Waislamu wana maadui wa kihistoria na kwamba Wazayuni ndio maadui wa mataifa yote ya Kiislamu. Amesisitiza kuwa Wazayuni hawayatakii mema mataifa yote ya Kiislamu.
Vilevile amewahimzia Waislamu kufaidika na baraka za mwezi huu mtukufu wa Ramadhani na kusema, kufanya ibada katika mwezi huu ambamo shetani amefungwa minyororo na milango ya rehma za Mwenyezi Mungu imefunguliwa, ni bora mara kadhaa kuliko kufanya ibada katika miezi mingine ya mwaka.

No comments: