Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

Annan: Baraza la Usalama linapaswa kurekebishwa

Katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa Kofi Annan amesisitiza ulazima wa kufanyiwa marekebisho muundo wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Annan amesisitiza kuwa, muundo wa hivi sasa wa Baraza la Usalama ni wa zamani, kwani unakidhi mahitaji yaliyokuweko katika muongo wa 90, hivyo unapaswa kubadilishwa.
Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kitabu chake huko Moscow nchini Russia, katibu mkuu wa zamani wa Umoja wa Mataifa amesema kuwa, India pamoja na kuwa na zaidi ya watu bilioni moja, haina kiti kwenye baraza hilo. Ameongeza kuwa, inashangaza kuona pia nchi za Kiafrika na zile za Amerika ya Latini nazo hazina kiti cha kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa.
Kuhusu mgogoro wa Syria, Kofi Annan ambaye aliwahi kuwa mjumbe wa Umoja wa Mataifa kwenye mgogoro wa nchi hiyo amesema kuwa, nchi zote wanachama wa Umoja wa Mataifa zinapaswa kuwa na sauti moja katika kuunga mkono mpango wa kufanyika mkutano wa kimataifa wa Geneva 2 wenye lengo la kuukwamua mgogoro wa Syria.

No comments: