Rooney Daniel mchambuzi wa masuala ya kijeshi wa utawala haramu wa
Kizayuni wa Israel, amefichua kuwa, Abdul Fatah as Sisi, Waziri wa
Ulinzi wa Misri, aliitaarifa Israel kuwepo njama za kumpindua Rais
Muhammad Morsi wa nchi hiyo siku tatu kabla ya tukio hilo. Akizungumza
kupitia kanali ya pili ya televisheni ya utawala huo, Rooney Daniel
amesema kuwa,
as Sisi aliutaka utawala wa Kizayuni kuimarisha ulinzi
dhidi ya Harakati ya Mapambano ya Kiislamu ya Palestina HAMAS kwa
kukhofia kuwa, inaweza kutoa radiamali kali dhidi ya Misri. Aidha
amesema kuwa, as Sisi aliwambia viongozi wa Tel Aviv kwamba, anaiogopa
harakati ya Hamas na Israel ilimuhakikishia waziri huyo wa ulinzi wa
Misri kwamba, itaweka ulinzi mkali katika mipaka ya Ukanda wa Ghaza ili
kuzuia hatua zozote zinazoweza kuchukuliwa na HAMAS. Kwa upande wake
utawala wa Kizayuni wa Israel ulimtaka as Sisi kuharibu njia za chini
kwa chini zinazotumiwa na wakazi wa Ukanda wa Ghazas mkabala na ulinzi
huo wa Israel. Daniel amefafanua zaidi kuwa, mapinduzi ya kijeshi dhidi
ya Mursi, ni kwa maslahi ya utawala wa Kizayuni wa Israel na ni katika
kuudhaminia usalama utawala huon ghasibu.
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
No comments:
Post a Comment