Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Wednesday, July 17, 2013

22 wauawa mashambulio ya NATO Afghanistan

Kwa akali watu 22 wameuawa nchini Afghanistan na makumi ya wengine kujeruhiwa kufuatia mashambulio mawili tofauti ya anga yaliyofanywa na majeshi ya NATO nchini humo. Taarifa zaidi zinasema kuwa, vikosi vya Jumuiya ya Kijeshi ya NATO vimefanya mashambulio makubwa katika majimbo ya Paktia na Ghazni na kusababisha mauaji hayo.
Msemaji wa Gavana wa jimbo la Ghazni Nabil Jan amesema kuwa, raia 10 wameuawa katika shambulio lililofanywa na vikosi vya NATO katika kijiji cha Khogian. Wakati huo huo, Kamanda wa polisi wa jimbo la Paktia naye amethibitisha majeshi ya NATO kufanya mashambulio katika jimbo hilo na kuongeza kuwa, watu wasiopungua 12 wameuliwa katika shambulio hilo. Ameongeza kuwa, mji uliolengwa na mashambulio hayo ya NATO katika jimbo la Paktia ni wa Zarmat.

No comments: