Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 21, 2013

Wapinzani Ethiopia wapinga 'sheria dhidi ya ugaidi'

Chama kikuu cha upinzani Ethiopia kimetoa wito kwa serikali ya nchi hiyo kufuta sheria dhidi ya ugaidi ambayo imekuwa ikitumiwa kuwakandamiza wapinzani.  Msemaji wa Chama cha Unity for Democracy and Justice Daniel Tefera amesema iwapo sheria hiyo haitabatilishwa wataitisha maandamano makubwa kama yale yaliyoshuhudiwa mjini Addis Ababa mapema mwezi huu.

Sheria dhidi ya ugaidi iliyopitishwa nchini humo mwaka 2009 inaonekana kuwasakama zaidi wapinzani wa serikali kwa sababu kila atakayeshapisha taarifa ambazo zinaonekana kuchochea ghasia anaweza kuhukumiwa kifungo cha baina ya miaka 10 hadi 20 jela. Hadi sasa waandishi habari 10 wamefikishwa mahakamani kwa msingi wa sheria hiyo dhidi ya ugaidi.
Serikali ya Ethiopia inasema sheria hiyo ni muhimu katika kukabiliana na waasi wanaotaka kujitenga ambao wanaoungwa mkono na nchi jirani ya Eritrea.

No comments: