Leo ni Ijumaa tarehe 12 Shaaban mwaka 1434 Hijria sawa na tarehe 21 Juni 2013 Miladia.
Siku kama ya leo miaka 32 iliyopita sawa na tarehe 31 Khordad 1360
Hijria Shamsia, aliuawa shahidi Dakta Mustafa Chamran, msomi na kamanda
shujaa wa vikosi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wakati wa vita vya
kulazimishwa vilivyoanzishwa na Iraq dhidi ya Iran. Dakta Chamran
alifanikiwa kupata shahada katika fani ya elektroniki na kisha akaelekea
Marekani ambako alifanikiwa kupata shahada ya uzamivu yaani PhD. Kwa
miaka kadhaa Dakta Chamran alikuwa nchini Lebanon kwa ajili ya
kuwasaidia wananchi wa nchi hiyo waliokuwa wakipambana na utawala wa
Kizayuni wa Israel. Mara baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu Dakta
Chamran alichaguliwa kuwa Waziri wa Ulinzi wa Iran na kisha akawa
mbunge wa Tehran. Baada ya kuanza mashambulizi ya Iraq dhidi ya Iran,
dakta Chamran alijiunga na wanapambano na kuongoza operesheni nyingi
katika vita hivyo.
Sambamba na kushiriki katika mstari wa mbele vitani,
Chamran alikuwa malenga na arif na ameacha maandishi mengi. Hatimaye
aliuawa shahidi akiwa vitani na baada ya kufikia daraja hiyo ya juu Imam
Khomeini MA alitoa ujumbe maalumu na kusema alikuwa shakhsia mwenye
ikhlasi na aliyejitolea katika Jihadi kwa akili ya Allah SWT.
Miaka 43 iliyopita katika siku kma ya leo inayosadifiana na tarehe 21
Juni 1970, alifariki dunia Dakta Ahmed Sukarno kiongozi wa mapambano ya
kupigania uhuru wa Indonesia. Sukarno alizaliwa mwaka 1901, na alikuwa
mstari wa mbele katika mapambano yake dhidi ya mkoloni Mholanzi nchini
humo. Kwa minajili hiyo, Sukarno aliwahi kukamatwa na kufungwa jela kwa
miaka minne na utawala wa kikoloni wa Uholanzi. Baada ya kifungo hicho
aliwahi kutiwa tena mbaroni na kubaidishwa. Mnamo mwaka 1949
alichaguliwa kuwa Rais wa Indonesia na ilipofika mwaka 1965 Ahmed
Sukarno akaondolewa madarakani baada ya kufanyika mapinduzi ya kijeshi
yaliyoongozwa na Jenerali Suharto.
Na siku kama ya leo miaka 23 iliyopita, inayosadifiana na 31 Khordad
1369 Hijria Shamsia, mikoa ya Gilan na Zanjan iliyoko kaskazini na
kaskazini magharibi mwa Iran ilikumbwa na mtetemeko mkubwa wa ardhi
uliosababisha maafa makubwa. Zaidi ya watu elfu hamsini walifariki
dunia, wengine zaidi ya elfu sitini kujeruhiwa na laki tano kukosa
makaazi. Mtetemeko huo licha ya kuleta maafa kwa binadamu, ulisababisha
hasara kubwa ya kiuchumi kwa wananchi na serikali.
No comments:
Post a Comment