Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Friday, June 21, 2013

Makamu wa rais wa Sudan Kusini kuelekea Khartoum

Makamu wa Rais wa Sudan Kusini Riek Machar atatembelea mji mkuu wa Sudan, Khartoum wiki ijayo. Shirika la Habari la Sudan SUNA limesema Machar atafanya ziara hiyo wiki ijayo baada ya safari iliyokuwa imepangwa Jumapili wiki hii kuakhirishwa kwa sababu baadhi ya mawaziri wa Sudan walikuwa nje ya nchi. Serikali ya Sudan Kusini awali ilikuwa imetangaza kuwa Machar ataenda Khartoum kujaribu kutatua mgogoro wa mafuta baina ya nchi mbili.

Uhusiano wa pande mbili hizo ulizorota mwezi huu pale Sudan iliposema itazuia mafuta ya Sudan Kusini kupita katika ardhi yake iwapo wakuu wa Juba hawatasitisha uungaji mkono wao kwa waasi wanaoipinga serikali ya Khartoum. Sudan Kusini inategemea mabomba ya Sudan kuuza mafuta yake katika masoko ya kimataifa.
Mashirika ya mafuta ya China, India na Malaysia ambayo hununua mafuta ya Sudan Kusini yanapata hasara kubwa kutokana na mzozo baina ya nchi hizo mbili.

No comments: