Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Wanaharakati wa haki za binaadamu mjini Istanbul

Mamia ya wanaharakati wa kutetea haki za binaadamu mjini Istanbul, Uturuki, wamefanya maandamao dhidi ya serikali ya nchi hiyo. Wanaharakati hao walimiminika mabarabarani jana huku wakitoa nara za kupinga siasa za kidikteta za Recep Tayyip Erdoğan Waziri Mkuu wa nchi hiyo. Aidha waandamanaji hao walielekea kwenye medani ya Taksim na kulaana siasa za ukandamizaji zinazotekelezwa na polisi ya nchi hiyo dhidi ya waandamanaji. Kabla ya hapo pia, maelfu ya wakazi wa mjini Istanbul walikusanyika katika medani hiyo na kutoa nara za kupinga serikali inayoongozwa na Erdogan.
Ni vyema kuashiria hapa kuwa, tangu tarehe 31 Mei nwaka huu, Uturuki imekuwa ikishuhudia wimbi kubwa la maandamano ya wananchi dhidi ya serikali. Mbali na waandamanaji kupinga hatua ya kutaka kuharibu bustani ya Gezi, wanalaani vikali pia msimamo wa Erdogan wa kuunga mkono magaidi wanaotaka kuiangusha serikali ya wananchi wa Syria. Waturuki sasa wanataka Waziri Mkuu Erdogan ajiuzulu na kuitishwa uchaguzi wa mapema nchini humo.

No comments: