Social Icons

twitterfacebookgoogle pluslinkedinrss feedemail

Tuesday, June 25, 2013

Chadema: CCM inataka kutubambikizia kesi

Chama Kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, kimekituhumu chama tawala cha CCM kuwa, kina mpango mchafu wa kuwabambikizia viongozi wakuu wa chama hicho kesi ya kumwagiwa Tindikali kada wa Chama Cha Mapinduzi CCM, Musa Tesha. Chadema kimeongeza kuwa, Viongozi wanaoandaliwa mpango huo ni pamoja na Mwenyekiti wa chama hicho, Freeman Mbowe, Katibu Mkuu, Dakta. Willibrod Slaa, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Ubungo, John Mnyika.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Habari na Uenezi wa Chadema, Mnyika, wakati akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam, na kuongeza kuwa, mpango huo unafanyika kwa lengo la kukidhoofisha chama chao kinachowapa wakati mgumu CCM. Aidha Mnyika amesema, hivi sasa makachero wa polisi wamekuwa wakiwakamata vijana na kuwalazimisha kukiri kwa kuandika au kuandikiwa maelezo kuwa viongozi hao waliwatuma kummwagia tindikali Tesha wakati wa uchaguzi mdogo wa Igunga mwaka 2011. Alibainisha kuwa, kutokana na kesi hiyo kuonekana kujaa masuala ya kisiasa, kitashirikiana na mawakili wake kwa ajili ya kukabiliana na njama hiyo.

No comments: